Yesu Kwetu Ni Rafiki
[1]
Yesu kwetu ni rafiki,
Huambiwa haja pia
Tukiomba kwa babaye
Maombi asikia;
Lakini twajikosesha,
Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu
Dua angesikia
[2]
Una dhiki na maonjo?
Una mashaka pia?
Haifai kufa moyo,
Dua atasikia
Hakuna mwingine mwema
Wa kutuhurumia;
Atujua tu dhaifu;
Maombi asikia
[3]
Je, hunayo hata nguvu
Huwezi kwendelea,
Ujapodharauliwa
Ujaporushwa pia
Watu wangekudharau,
Wapendao ndunia,
Hukwambata mikononi
Dua atasikia.
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.