Ni Tabibu Wa Karibu
[1]
Ni tabibu wa karibu
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima
Ni dawa yake njema
[chorus]
Imbeni malaika, sifa zaYesu Bwana
Pweke limetukuka, jina lake Yesu
[2]
Hatufai kuwa hai
Wala hatutumai
Ila yeye kweli ndiye
Atupumzishaye.
[chorus]
Imbeni malaika, sifa zaYesu Bwana
Pweke limetukuka, jina lake Yesu
[3]
Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia
Twenendeni na amani
Hata kwake mbinguni
[chorus]
Imbeni malaika, sifa zaYesu Bwana
Pweke limetukuka, jina lake Yesu
[4]
Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana
Yu na sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa
[chorus]
Imbeni malaika, sifa zaYesu Bwana
Pweke limetukuka, jina lake Yesu
[5]
Kila mume asimame
Sifa zake zivume
Wanawake na washike
Kusifu jina lake
[chorus]
Imbeni malaika, sifa zaYesu Bwana
Pweke limetukuka, jina lake Yesu
[6]
Na vijana wote tena
Wampendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake.
[chorus]
Imbeni malaika, sifa zaYesu Bwana
Pweke limetukuka, jina lake Yesu
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.