Kazi Yangu Ikiisha
[1]
Kazi yangu ikiisha, nami nikiondoka,
Na kuvaa kutokuharibika,
Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni,
Atakuwa wa kwanza kunilaki.
[chorus]
nitamjua , nitamjua nikimwona uso kwa uso,
Nitamjua,nitamjua kwa alama za misumari
[2]
Furaha nitapata nikiona makao
Bwana aliotuandalia
Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo
Vilivyonipa pahali Mbinguni
[3]
Naowaliokufa katika Bwana Yesu
nitawaona tena huko juu
Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni
Nataka kumwona Mwokozi kwanza.
[4]
Milangoni mwa mji Bwana atanipisha
Pasipo machozi wala huzuni
Nitaimba wimbo wa milele; lakini
Nataka kumwona Mwokozi kwanza
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.