Wamwendea Yesu Kwa Kusafiwa
[1]
Wamwendea Yesu kwa kusafiwa,
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Je, neema yake umemwagiwa?
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
[2]
Wamwandama daima Mkombozi
Na kuoshwa kwa damu ya kondoo?
Yako kwa Msulubiwa makazi,
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
[3]
Atakaporudi Bwana arusi
Uwe safi kwa damu ya kondoo!
Yafae kwenda Mbinguni mavazi
Yafuliwe kwa damu ya kondoo?
[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
[4]
Yatupwe yalipo na takataka,
Na uoshwe kwa damu ya kondoo
Huoni kijito cha tiririka
Na uoshwe kwa damu ya kondoo?
[chorus]
Kuoshwa, kwa damu
Itutakasayo ya kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe mno;
Umeoshwa kwa damu ya kondoo?
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.