Waimba Sikizini
[1]
Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni,
Wimbo wa tamu sana, wa pendo zake Bwana,
"Duniani salama, Kwa wakosa rehema"
Sisi sote na twimbe, nao wale wajumbe,
Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni
[2]
Ndiye Bwana wa mbingu, Tangu milele Mungu,
Amezaliwa mwili, Mwana wa mwanamwili;
Ametoka enzini, Kuja ulimwenguni
Mwokozi atufie, ili tusipotee
Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni.
[3]
Seyidi wa amani, Ametoka mbinguni,
Jua na haki, ndiye atumulikiaye
Amejivua enzi, Alivyo na mapenzi
Ataka kutuponya, Kutuzalisha upya,
Waimba, sikizeni, Maliika mbinguni
[4]
Njoo upesi, Bwana, Twakutamani sana;
Kaa nasi, Mwokozi, Vita hatuviwezi,
Vunja kichwa cha nyoka, Sura zako andika,
Tufanane na Wewe, Kwetu sifa upewe
Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni.
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.