Nimelemewa Na Hatia Zangu
[1]
Nimelemewa na hatia zangu
Nakutamani kufikia mbingu
Ingawa mwenye dhambi haingii
Iko sauti yaniita nije.
[chorus]
(Naja) Naja kwako Yesu Bwana
(Nisa) Nisafiwe dhambi zangu X2
[2]
Mimi mchafu nitaweza wapi
Kufika kwenye nchi takatifu
Kitini kwa mwamuzi nisimame
Uko mkono wanivuta nije.
[chorus]
(Naja) Naja kwako Yesu Bwana
(Nisa) Nisafiwe dhambi zangu X2
[3]
Ingawa natamani kufuata
Njia ya haki dhambi zanipinga
Lakini nasikia neno njema
Tubu ungama utasamehewa.
[chorus]
(Naja) Naja kwako Yesu Bwana
(Nisa) Nisafiwe dhambi zangu X2
[4]
Sauti yako Yesu nasikia
Mikono yake yanivuta leo
Na damu yako yanisafisha dhambi
Na kuniweka safi mbele yako.
[chorus]
(Naja) Naja kwako Yesu Bwana
(Nisa) Nisafiwe dhambi zangu X2
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.