Mwokozi Moyoni Mwangu
[1]
Tangu siku hiyo aliponijia
Akae moyoni mwangu
Sina giza tena ila mwanga pia
Kwa Yesu mwokozi wangu
[chorus]
Amani moyoni mwangu
Kwa Yesu mwokozi wangu
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye
Yu nami moyoni mwangu.
[2]
Sina haja tena ya kutangatanga
Ndiye kiongozi wangu
Dhambi zangu zote zimeondolewa
Kwa Yesu Mwanawe Mungu
[chorus]
Amani moyoni mwangu
Kwa Yesu mwokozi wangu
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye
Yu nami moyoni mwangu.
[3]
Matumaini yangu ni ya hakika
Katika mwokozi wangu
Hofu yangu na hamu zimeondoka
Kwa kuwa ninaye Yesu.
[chorus]
Amani moyoni mwangu
Kwa Yesu mwokozi wangu
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye
Yu nami moyoni mwangu.
[4]
Siogopi tena nikiitwa kufa
Yu nami daima Yesu
Mlango wa mbinguni ni yeye pia
"Tapita humo kwa damu".
[chorus]
Amani moyoni mwangu
Kwa Yesu mwokozi wangu
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye
Yu nami moyoni mwangu.
[5]
Nitaketi na Yeye huko milele
Nisifu mwokozi wangu
Nina raha moyoni majira yote
Kwa Yesu Mwanawe Mungu.
[chorus]
Amani moyoni mwangu
Kwa Yesu mwokozi wangu
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye
Yu nami moyoni mwangu.
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.