SAUTI NI YAKE BWANA
[1]
Sauti ni yake Bwana, ‘Kwenda nani tayari?‘
Mavuno yanakawia, Nani atayavuna?
Kwa kudumu anaita, Zawadi atatoa;
Nani atakayejibu, ‘Nipo Bwana nitume.‘
[2]
Kama huwezi safari, Hata nchi za mbali,
Pana watu karibuni, Wasiomjua Yesu;
Kama huwezi kusema, Jinsi ya malaika,
Waweza kuutangaza, Upendo wa Mwokozi.
3
Ingawa huwezi kuwa, Mkesha mlangoni,
Ukiwatolea watu, Nafasi ya uzima;
Kwa sala na kwa sadaka, Watoa msaada,
Kama Harun mwaminifu, Kuinua mikono.
[4]
Roho za watu zikifa, Bwana akikuita,
Usiseme kwa uvivu, ‘Hakuna kazi kwangu‘.
Kwa furaha anza kazi, Ile aliyokupa,
Ukajibu mara moja, ‘Nipo Bwana nitume‘.
10[7]
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.