PENDO LAKO, EE MWOKOZI
[1]
Pendo lako , Ee Mwokozi, Hushinda pendo zote!
Kaa nasi, ndani yetu, Furaha ya mbinguni.
Yesu, u rehema tupu, Safi, na kusamehe,
Mfariji mwenye huzuni Ziondoe machozi.
[2]
Roho yako ya upendo Tuma kwa kundi lako;
Hebu tuirithi raha, Iliyoahidiwa.
Uondoe moyo mbaya, U Mwanzo, tena Mwisho;
Timiza imani yetu, Ilituwekwe `huru.
[3]
Yesu, uje kwetu sasa, Tupokee huruma;
Rudi kwetu, tena kamwe Usituache pekee.
Tungekutukuza leo, pamoja na malaika,
Imba na kutoa sifa, Ingia kwa ibada.
[4]
Sasa, Bwana, kazi yako, Imalize moyoni;
Takasa hekalu lako, Wokovu kamilisha!
Safisha viumbe vyako Katika wakati huu;
Tupumzike `toka dhambi, Tuingie mbinguni.
03[7]
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.