HUNA KITU KWA YESU
[1]
Ukitafuta mali, Huna wasaa kwa Yesu?
Kwa matendo ya haki Huna wasaa kwa Yesu?
Anasa za dunia, Mambo yako ya raha
Haya unatafuta; Huna wasaa kwa Yesu?
[2]
Mambo yanakusonga: Kwakehuna nafasi?
Watekwa na dunia, Kwake huna nafasi?
Humwona m-langoni, Anapopiga hodi?
Daima hukusihi: Kwake huna nafasi?
[3]
Sa-a ni za thamani, Kwake hamnayo kazi
Wala hamfanyi bidii, Kwake hamnayo kazi?
Hamkufikia kwao Waliomo shimoni
Na waliopotea? Kwake hamnayo kazi?
[4]
Na wazaa majani tu? Huna tunda kwa Yesu?
Mikono I mitupu, Huna tunda kwa Yesu?
Huna chembe kwa ghala Kazi yako kulipa;
Wala huna furaha Unapomwona Yesu?
10[6]
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.