Bwana, Nitume
[1]
Sauti ni yake Bwana, “Kwenda, nani tayari”
Mavuno yanakawia, Nani atayavuna?
Kwa kudumu amaita, Zawadi atatoa;
Nani atakayejibu “Nipo Bwana, nitume.”
[2]
Kana huwezi safari Hata Nchi za mbali,
Pana watu karibuni Wasio mjua Yesu;
Kama huwezi kusema Jinsi ya malaika,
Waweza kuutangazaUpendo wa mwokozi.
[3]
Ingawa huwezi kuwa Mkesha mlangoni,
Ukiwatolea watu Nafasi ya uzima;
Kwa sala na kwa sadaka Watoa msaada,
Kama Harun mwaminifu,Kuinua Mikono.
[4]
Roho za watu zikifa, Bwana akikuita,
Usiseme kwa uvivu, “Hakuna kazi kwangu.”
Kwa furaha anza kazi Ile akiyokupa,
Ukajibu mara moja “nipo Bwana, nitume.”
Support Mysongbooks
Support us by joining the Buy Me A Coffee community and making a small donation, you can help us expand our library and ensure that music lovers everywhere can enjoy their favorite songs to the fullest. We're passionate about music, and we know you are too, so let's work together to keep the music alive.
Thank you for being a part of our community and supporting our mission to provide the best lyrics library on the internet.